UKIRI WA NENO LA MUNGU

UKIRI WAKO NDIO USHINDI WAKO



K
umwona Mungu akitenda katika maisha yako inategemea ni kwa namna gani na mtizamo gani ulionao juu ya neno la MUNGU. Je, unalichulia NENO la MUNGU kama ahadi tu zilizo andikwa kwenye kitabu (BIBLIA)? Au Kama NENO hai litokalo kinywani mwa MUNGU likiwa na nguvu zake kufanya matendo makuu maishani mwako?

WAEBRANIA 4:12
“12 Maana Neno la Mungu li hai, tena lina nguvu, tena lina ukali kuliko upanga uwao wote ukatao kuwili, tena lachoma hata kuzigawanya nafsi na roho, na viungo na mafuta yaliyomo ndani yake; tena li jepesi kuyatambua mawazo na makusudi ya moyo.”

Neno la MUNGU siku zote ni jipya kila siku, lina nguvu na linatenda kazi kama enzi zile za zamani, halijawai pungua nguvu. MUNGU analitukuza NENO lake kuliko jina lake (ZABURI 138:2). 
Kazi ipo kwetu kulitendea kazi NENO kwa namna tunavyotaka iwe maishani mwetu. Na hii inafanyika kwa namna tunavyolikiri NENO la MUNGU katika maisha yetu ya kila siku. Kukiri kwako kunakutengenezea hamasa Fulani na nguvu ya kipekee Moyoni mwako ya kuona kuwa mambo yananenda kukaa sawa haijalishi ni hali gani unaipitia.
Kusikia, Kuamini, na Kukiri Neno la MUNGU kutakufanya kuwa mtu wa kubadilisha hali na mazingira na si mazingira kukubadilisha wewe.  Tunamuona mwanadamu wa kwanza ADAM alivyotambua kuwa kuna nguvu katika kutamka Neno, alianza kubadilisha mazingira. Alianza kuwapa viumbe majina, kila mnyama wa kufugwa na ndege wa Angani na kila mnyama wa polini wote walipewamajina (MWANZO 1:20)…  Biblia haitwambii kuwa Mungu alimwambia Adamu awape viumbe majina lakini Automatically Adam alianza kuwapa viumbe majina.
Kuna nguvu ya kipekee katika kutamka na kutabiri kwa kutumia vinywa vyetu. Ndo maana nipenda sana kusema “KUKIRI KWAKO KATIKA IMANI NDIO USHINDI WAKO”

ISAYA 55:10-11
"10 Maana kama vile mvua ishukavyo, na theluji, kutoka mbinguni, wala hairudi huko; bali huinywesha ardhi, na kuizalisha na kuichipuza, ikampa mtu apandaye mbegu, na mtu alaye chakula;
 11 ndivyo litakavyokuwa neno langu, litokalo katika kinywa changu; halitanirudia bure, bali litatimiza mapenzi yangu, nalo litafanikiwa katika mambo yale niliyolituma."

BIBLIA inavyo vitabu 66 vilivyojaa sheria/maagizo, na ahadi za MUNGU zilizo kuu. KAZI WETU KUTENDEA KAZI NENO

IMANI na MATOKEO YA IMANI vinategemea namna kanuni hii inavyofanyiwa kazi……………………………………….

KUSIKIA NENO LA MUNGU -àKUAMINI -àKUKIRI NA KUTENDEA KAZI NENO

Kusikia kuwa YESU anaponya haitoshi tu kwako wewe kupata uponyaji. Kuamini tu moyoni mwako kuwa YESU anaponya haitoshi tu kwako kupokea uzima mpaka pale utakapochukua jukumu la kukiri kile NENO linamaanisha, pale utakapotendea kazi NENO la MUNGU kile linachokuagiza au Kulitamka kama vile ni lakwako.

Kwa mfano: NENO la MUNGU linasema

 KUMBUKUMBU LA TORATI  28
"13 BWANA atakufanya kuwa kichwa, wala si mkia; nawe utakuwa juu tu, wala huwi chini; utakapoyasikiza maagizo ya BWANA, Mungu wako, nikuagizayo hivi leo, kuyaangalia na kufanya;"
Kuwa kichwa sio tu pale utakapoamini kuwa wewe utakuwa kichwa bali ni pale utakapokiri kwa kinywa chako kuwa "Mimi ni kichwa Na wala sio mkia, nitashinda katika kila jambo nifanyalo, nitapiga hatua kwa sababu Mungu wangu ndiye anipaye kushinda; ninakataa kufeli. Na kufeli kuwa mkia, kuchoka, kukata tamaa, kufadhaika, na kuugua hakuna nafasi kwangu”
Huo ni mfano wa ni kwa namna gani MTU anaweza kukiri ahadi za Mungu Na kushuhudia matendo makuu ya MUNGU. Imani bila matendo imekufa....
Imetupasa kulitendea kazi NENO la MUNGU, Kukiri hasa kile MUNGU ametuahidi. Tusishikilie mabango yenye ahadi mioyoni mwetu, Bali tuzikiri hizo ahadi Na kuzifanya na kuzifanya kuwa zetu.
Kuna vielelezo vingi vya kuthibitisha kuwa KUKIRI na kufanya kile ulichoagizwa na Neno la MUNGU ndio muujiza mkuu wa kumwona MUNGU akifanya kwa ajili Na kuyaona mambo yakitokea automatically kwa sababu wewe unayo mamlaka kuu.
Mara nyingi tumekuwa watu wa kutumia vinywa Na maneno yetu ndivyo sivyo, na kuliacha pembeni jukumu kubwa na lenye maana la kuzikiri ahadi za Mungu kana kwamba ni zetu.

MITHALI 12:14
"14 Mtu atashiba mema kwa matunda ya kinywa chake;Na atarudishiwa matendo ya mikono yake."
Ukikitumia kinywa chako hasa katika kikiri Na kulitendea kazi
NENO la MUNGU Hakika lazima ule matunda ya midomo yako kwa sababu umejua kutuma kinywa vizuri katika kujitabiria mema.

Iko mifano yakutosha katika kuthibitisha kwa kina kile ambacho tunapaswa kukiri na kufanya kulingana na kile tunachoagizwa na NENO la MUNGU.

 Mfano mojawapo ni……………………. Wa kutoka kitabu cha EZEKIELI

EZEKIELI 37:3-10
"3 Akaniambia, Mwanadamu, je! Mifupa hii yaweza kuishi? Nami nikajibu, Ee Bwana MUNGU, wajua wewe.
4 Akaniambia tena, Toa unabii juu ya mifupa hii, uiambie, Enyi mifupa mikavu, lisikieni neno la BWANA.
5 Bwana MUNGU aiambia mifupa hii maneno haya; Tazama, nitatia pumzi ndani yenu, nanyi mtaishi.
6 Nami nitatia mishipa juu yenu, nami nitaleta nyama iwe juu yenu, na kuwafunika ngozi, na kutia pumzi ndani yenu, nanyi mtaishi; nanyi mtajua ya kuwa mimi ndimi BWANA.
7 Basi nikatoa unabii kama nilivyoamriwa; hata nilipokuwa nikitoa unabii, palikuwa na mshindo mkuu; na tazama, tetemeko la nchi, na ile mifupa ikasogeleana, mfupa kwa mfupa mwenziwe.
8 Nikatazama, kumbe! Kulikuwa na mishipa juu yake, nyama ikatokea juu yake, ngozi ikaifunika juu yake; lakini haikuwamo pumzi ndani yake.
9 Ndipo akaniambia, Tabiri, utabirie upepo, mwanadamu, ukauambie upepo, Bwana MUNGU asema hivi; Njoo, kutoka pande za pepo nne, Ee pumzi, ukawapuzie hawa waliouawa, wapate kuishi.
10 Basi nikatabiri kama alivyoniamuru; pumzi ikawaingia, wakaishi, wakasimama kwa miguu yao, jeshi kubwa mno."

Ezekieli alipoulizwa kama mifupa inaweza kuwa hai hakushangaa maana alijua kuwa MUNGU ndiye awezaye kufanya vitu kuwa hai kwahiyo hill halimshindi. Lakini kuamini kuwa MUNGU anaweza kufanya hivo halikuifanya mifupa iweze kuwa Hai, isipokuwa nni pale tu alipoamua kufanya kama alivyoagizwa Na Bwana MUNGU kutoa unabii juu ya mifupa kuwa hai.
Nasi kwa vinywa vyetu tunayo nafasi ya kutabiri au kutoa unabii juu ya maisha yetu Na kujinenea mambo mwema kwa kuzikiri ahadi za MUNGU mwetu kwa sababu, ahadi zote za MUNGU zimetimilika ndani ya Kristo.

WAKOLOSAI 1:19
"19 Kwa kuwa katika yeye ilipendeza utimilifu wote ukae;"
Nasi kwa sababu ttumefananishwa Na Kristo mwenyewe basi Ahadi zote za MUNGU zimetimilika ndani yetu kwa sababu Kristo anaishi ndani yetu.

Na sisi sio watu wa kawaida, ni watu wa Milki ya MUNGU Ukuhani ufalme Na tupate kuzitangaza fadhiri za MUNGU, Na MUNGU mwenyewe ajidhihirishwa kwa walimwengu kupitia sisi, kama alivyojidhihirisha kwa wanadamu Kupitia Kristo YESU mwana wake.

      SALA
BABA katika jina la YESU KRISTO aliye Hai, ninakushukuru kwa jinsi ulivyonikirimia Ahadi kubwa mno, ninashukuru kwa sababu nimeumbwa kwa mfano wako, na ndani yangu imo nguvu yako kwa sababu unaishi ndani yangu. Ninakiri kuwa mimi ni mshindi kwa sababu Kristo YESU Bwana wetu ameushinda ulimwengu. Nimebarikiwa na nitazidi kubarikiwa kwa sababu ahadi zako ni Kweli na Amina, wewe hubadiliki na wala NENO lako halitokuja kutanguka. Ninakiri kuwa kwangu hakuna magonjwa, hakuna kufeli, hakuna madhaifu wala mahangaiko. Kila ulichokwisha kuahidi kwangu hakika kinaenda kutimia katika jina la YESU. Ninahitaji Neema yako iendelee kuwa pamoja nami siku zote niyashuhudie matendo yako makuu maishani mwangu. Ili watu wengine wajue hakika ya kuwa wewe ndiwe MUNGU pekee yako na wala hakuna Mwingine. Sifa, utukufu, adhama, mamlaka na enzi vina wewe BABA wa MBINGUNI.

BY: MWL. GEORGE JOHN 
GOSPEL MINISTRY
(Turning souls to christ)

Comments

Popular posts from this blog

USHUHUDA WA MBINGUNI NA KUZIMU