Popular posts from this blog
UKIRI WA NENO LA MUNGU
UKIRI WAKO NDIO USHINDI WAKO K umwona Mungu akitenda katika maisha yako inategemea ni kwa namna gani na mtizamo gani ulionao juu ya neno la MUNGU. Je, unalichulia NENO la MUNGU kama ahadi tu zilizo andikwa kwenye kitabu (BIBLIA)? Au Kama NENO hai litokalo kinywani mwa MUNGU likiwa na nguvu zake kufanya matendo makuu maishani mwako? WAEBRANIA 4:12 “12 Maana Neno la Mungu li hai, tena lina nguvu, tena lina ukali kuliko upanga uwao wote ukatao kuwili, tena lachoma hata kuzigawanya nafsi na roho, na viungo na mafuta yaliyomo ndani yake; tena li jepesi kuyatambua mawazo na makusudi ya moyo.” Neno la MUNGU siku zote ni jipya kila siku, lina nguvu na linatenda kazi kama enzi zile za zamani, halijawai pungua nguvu. MUNGU analitukuza NENO lake kuliko jina lake (ZABURI 138:2). Kazi ipo kwetu kulitendea kazi NENO kwa namna tunavyotaka iwe maishani mwetu. Na hii inafanyika kwa namna tunavyolikiri NENO la MUNGU katika maisha yetu ya kila siku. Kukiri kwako kun...
USHUHUDA WA MBINGUNI NA KUZIMU
Na. Rachael Mushala Disemba 2011, Bwana aliturudisha Kwake mimi na ndugu zangu. Ingawa baba yetu ni mchungaji, sisi wote tulikuwa tumerudi nyuma na kumuacha Bwana. Tulijifanya Wakristo mbele ya wazazi wetu na kanisa, lakini tuliishi maisha ya dhambi shuleni na wakati walipokuwa mbali na nasi. Tulidanganya na kutenda tuliyopenda. Lakini Mungu alifanya muujiza. Dada zangu wawili, kaka na mimi tukatubu na kumgeukia Mungu tena. Tulipojitoa tena kwa Mungu, tuliamua kumtafuta kwa maombi mazito. Tulitaka tuwe na uzoefu wa nguvu zake. Tulihisi kwamba kama tutamtafuta kwa bidii, atatujibu na kusema na sisi pia. Tulitaka sana ubatizo wa Roho Mtakatifu. Siku moja tulipokuwa tukiomba, mdogo wangu, Lois, aliyekuwa na miaka 10 wakati huo, alisema anaona malaika! Uwepo wa Roho Mtakatifu ulijaza chumba na mdogo wangu mwingine Zipporah akaanza kunena kwa lugha! Ilikuwa ajabu lakini mimi nilihisi nimeachwa kwa sababu ingawa tulikuwa tukiomba, kaka yangu na mimi hatukubatizwa na Roho Mt...
Comments
Post a Comment