SISI TU UZAO WA YESU KRISTO


Lakini Bwana aliridhika kumchubua; Amemhuzunisha; Utakapofanya nafsi yake kuwa dhabihu kwa dhambi, Ataona uzao wake, ataishi siku nyingi, Na mapenzi ya Bwana yatafanikiwa mkononi mwake (Isaya 53:10).
Roho Mtakatifu, akinena kupitia Nabii Isaya, alitoa unabii kuhusiana na
kuja kwake Masihi kama sadaka kwa ajili ya dhambi na kweli kwamba Ataona “uzao” Wake, ambao utaongeza siku Zake hapa duniani. Uzao waYesu ni Kanisa. Kupitia Kanisa, Bwana Yesu ameongeza siku Zake.Yesu alikuja ulimwenguni humu, akaishi katika ulimwengu huu, akaushinda ulimwengu, akafa, akazikwa, akafufuka, na kupaa juu mbinguni. Lakini maisha Yake yanaendelea leo hii hapa duniani kupitia sisi. Sisi ndio tunaoyaishi maisha yake hapa duniani sasa. Anaendelea kuishi, kupitia sisi (Kanisa). Matendo 1:1 inazungumza juu ya “…mambo yote aliyoanza Yesu kufanya na kufundisha.” Ambapo inamaanisha kazi Zake za kimiujiza na mafundisho Yake kuhusiana na Ufalme wa Mungu. Na unavyoendelea kusoma zaidi katika Kitabu cha Matendo, utagundua kwamba Bwana Yesu aliendelea kufundisha na kufanya mambo yale yale kupitia wale Mitume ambao alikuwa amewachagua. Wao pia (Mitume), waliwarithisha mafundisho hayo hayo kwa wengine, na mwishowe, imetufikia kila mmoja wetu; na itaendelea mpaka pale Yesu atakaporudi tena. Sisi tu mabalozi Wake, tukiendelea kufundisha mambo yale yale Aliyofundisha, na kufanya ishara Alizozifanya.
Isaya 53:8 inasema, “…Maana amekatiliwa mbali na nchi ya walio hai; Alipigwa kwa sababu ya makosa ya watu wangu.” Ulimwengu ulifikiri kwamba umemmaliza; badala yake umetokea wewe na mimi! Leo, pindi unapoenda mahali, Yesu anaonekana (anadhihirika kupitia wewe). Kila wakati jawa na mawazo na fikra kwamba Kristo anaishi kupitia wewe. Mtu yeyote yule anayehitaji kujua Yesu anaonekanaje anahitaji tu kukutazama wewe! Wewe ni mng’ao wa utukufu Wake, chapa halisi ya nafsi Yake, mshirika wa uzima Wake, na msambazaji wa pendo Lake, haki, na neema. Wewe ni mwakilishi Wake katika ulimwengu huu sasa.

Sala
Baba Mpendwa wa mbinguni, ninakushukuru sana kwa pendo na neema ambazo umenikirimia. Ahsante kwa kujidhihirisha katika ulimwengu kwa kupitia maisha yangu. Mimi ni mng’ao wa utukufu Wake, chapa halisi ya nafsi Yake na maisha yangu ni udhihirisho wa sifa na utukufu wa Mungu, katika Jina Lake Yesu. Amina.



Somo zaidi:

Wagalatia 3:16; Wagalatia 3:29; 2 Wakorinto 5:20

Comments

Post a Comment

Popular posts from this blog

USHUHUDA WA MBINGUNI NA KUZIMU